Jumamosi 6 Juni 2026 - 19:44
Wapinzani wa Palestina wapinga meli iliyobeba watalii wa Israeli nchini Ugiriki

Hawza/ Makundi yanayoiunga mkono Palestina pamoja na vyama vya wafanyakazi katika bandari ya Piraeus nchini Ugiriki yamefanya mkusanyiko wa maandamano, yakipinga kuingia kwa meli ya kitalii iitwayo “Crown Iris” iliyokuwa imewabeba watalii wa Israeli.

Kwa mujibu wa taarifa ya kitengo cha kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, kwa kunukuu Shirika la Habari la Anadolu, kufuatia wito wa Shirikisho la Wafanyakazi wa Bandari, baadhi ya vyama vya wafanyakazi na taasisi nyingine zinazounga mkono Palestina zilifanya maandamano katika bandari ya Piraeus nchini Ugiriki, ambapo washiriki walipinga kutia nanga kwa meli ya kitalii “Crown Iris” (Crown Iris) iliyokuwa imewabeba watalii wa Israeli.

Waandamanaji, wakirejelea kuendelea kwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Ghaza na Lebanon, walionesha msimamo wao dhidi ya safari na starehe za watalii wa Israeli nchini Ugiriki.

Meli ya kitalii “Crown Iris” iliyokuwa imetia nanga katika bandari ya Piraeus, karibu na Athens, mji mkuu wa Ugiriki, ilikabiliwa na upinzani kutoka kwa makundi yanayoiunga mkono Palestina.

Katika mkujumuiko huo, washiriki wakiwa wameshika bendera za Palestina walipaza sauti kwa kusema “Uhuru kwa Palestina” na kuonesha mabango yenye ujumbe wa “Hapana kwa watalii wa mauaji ya kimbari.”

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha